Sunday, November 25, 2012

MBINU ZA MAFANIKIO KWA WAFANYABIASHARA

KATIKA haya mabadiliko ya milenia mpya, wajasiriamali wameweza kujitofautisha na wafanyabiashara wakubwa ili kuwaridhisha wateja wao. Kuwa na ujuzi, ustadi na uwezo wa kupigania kupata bidhaa bora ni njia mahususi ya kufanikisha biashara. Hivyo basi, mjasiriamali au mfanyabiashara mkubwa anatakiwa kuwa na mipango mizuri na ya kitafiti kufanikisha hili, kwani huo ni ufunguo wa mafanikio. Mara nyingi mfanyabiasgara lazima awe mbunifu. Hivyo unatakiwa kuwa mfikiriaji mzuri wa kuuza bidhaa unazozivumbua. Ni muhimu kuongeza thamani katika bidhaa ulizo nazo na huduma zako. Unapokuwa mjasiriamali unatakiwa kuwa na uvumbuzi wa mawazo yanayofanana na biashara yako kwa kuongeza thamani au huduma. Kwa matokeo hayo wateja watagundua ubora wakati watakapoona uhalisia wa bidhaa ulizo nazo. Unapotaka kuwa mfanyabiashara wa kiwango cha kuthaminiwa inakubidi uwe mtawala mzuri na meneja aliyebobea. Uwe hodari katika kujifunza na kupata faida ya teknolojia mpya ili iweze kukusaidia kukuza biashara yako katika uchumi mpya. Kukamilisha teknolojia mpya katika biashara yako ni lazima, hivyo utaendelea kukuza na kuifanya iende na wakati. Uwe mwendelezaji anayelenga kuimarisha mtandao. Kujihusisha na wafanyabiashara wengine ni muhimu sana kwa kuwa itakusaidia katika ukuaji wa biashara yako. Pia kuwa mwangalifu kuimarisha mawasiliano uliyo nayo kwa wateja wako na kujenga mawasiliano mengine mapya ili uweze kuwa na mazingira ya kiushindani. Baadhi ya mbinu za kufanya mabadiliko mazuri katika biashara yako ni pamoja na uwazi, mpango wa kibiashara ulio wazi au unaoeleweka na utaalamu. Uwazi unahitajika katika biashara yako, hivyo ni muhimu kutozuia habari zozote muhimu na kuwa mkweli kwa wateja wako. Kuwa na mpango wa biashara inayoeleweka kunakufanya uweze kuimarisha ubora wa bidhaa na huduma, ili kufikia mahitaji ya wateja wako na kuwaridhisha. Mpango wako wa biashara mara zote uwe unauangalia na kuuimarisha uweze kuelewa mabadiliko na mahitaji ya wateja wako. Unatakiwa kuimarisha na kutathmini utaalamu ulio nao ili kuweza kufanya kilicho bora zaidi. Usisahau kwamba unahitaji kutoa muda ili kuzingatia eneo lako la utaalamu ulionao. Kumbuka matangazo na masoko kwa biashara ndogo yanaongeza bidii na mipango ya kukuwezesha kufanikiwa zaidi. Wamiliki wengi wa biashara ndogo ndogo wanavunjwa moyo kwa haraka kwa sababu hawaelewi upepo wa biashara kwa wateja wao wanaowategemea baada ya kufanya kampeni ya matangazo yao ya awali. Matangazo ni sanaa inayokuwezesha kutazama na kutengeneza mpango wa muda mrefu utakaokuongoza katika mafanikio. Kuna mambo matatu wamiliki wa biashara ndogo ndogo wanayoweza kufanya katika kuongeza nafasi ya mafanikio katika kampeni ya kutangaza. Kwanza, unatakiwa kujiaminisha katika mpango wako wa muda mrefu. Kama hukufanya hivyo bilashaka unahitaji mpango mwingine. Jambo jingine ni kuwa unapokuwa na mipango ya kufungua biashara ni matangazo. Kujitangaza ni njia moja nzuri sana, lakini nayo inahitaji kuwe na hiyo mipango ya kujitangaza. Angalau unatakiwa kuwa na mpango wa kutangaza biashara zako kwa miezi sita, lakini ukweli ni kwamba inatakiwa ujitangaze kwa mwaka mzima. Hii itakusaidia kuimarisha mkataba wa muda mrefu na watangazaji, kwani kwa kufanya hivyo utakuwa unapunguza gharama za uangazaji. Hii inakusaidia kufikia ukomo uliojiwekea wa uchapaji na kutoa ujumbe mbalimbali unaotaka uwafikie wateja wako katika vipindi mbalimbali vya mwaka. Na jambo la tatu ni ongezeko la thamani - kama biashara ndogo unashindana na ushirika wa wateja wako. Unatakiwa kuwa tofauti. Zungumza kutokana na kile wateja wako wanachokihitaji na jinsi ya kuwapatia, lakini pia unaweza kuwa sehemu ya wateja. Inaweza kukuvunja moyo wakati unashindana na biashara ndogo na kubwa endapo hutapata matokeo mazuri ya biashara kutokana na ulivyojitangaza. Ili kuleta utofauti unayo nafasi kubwa ya kupata wateja wote ambao hawakufanyi ukatulia. Pata faida kwa kutoa huduma za bure – huduma za kawaida ambazo wafanyabiashara wadogo wanashindwa kufaidika nazo ni kutoa taarifa kwa vyombo vya habari. Kama una bidhaa mpya au huduma au kitu chochote kipya katika kiwanda chako ambacho unafikiri kuwa wateja wako wanatakiwa kujua, andika taarifa kwa vyombo vya habari. Pia unaweza kutoa taarifa hiyo kwenye magazeti binafsi.

No comments:

Post a Comment