Sunday, November 25, 2012

Njia 10 za kuimarisha kumbukumbu kichwani

Miongoni mwa hazina muhimu kwa mwanadamu ni kuwa na uwezo wa kukumbuka vitu kwa urahisi. Wanafunzi wengi hushindwa kufanya vizuri mitihani yao kwa sababu ya kukabiliwa na tatizo la usahaulifu, ambao huchochewa na mambo mengi ukiwemo ulevi wa pombe, utumiaji wa dawa za kulevya na msongo wa mawazo ya kimaisha. Licha ya uwezo wa kumbukumbu kupungua kutokana na umri wa mtu, sayansi yaitegemei kijana mwenye umri wa chini ya miaka 28 kukabiliwa na tatizo hili kwa kiwango kikubwa, ingawa wale wenye miaka zaidi ya 40 wanatajwa kuzorota katika uwezo wa kukumbuka mambo. Hata hivyo uchunguzi unaonesha kuwa watu ambao huzingatia suala la kanuzi za afya zikiwemo mbinu za kukuza kumbukumbu ya akili hupunguza kwa kiasi kikubwa mmeng�enyeko wa seli zinazojenga uwezo wa akili katika kutunza kumbukumbu. (Susan Tapert mwanasaikolojia kutoka Chuo cha California San Diego na kituo cha VA San Diego nchini Marekani anathibitisha haya pia). Hivyo basi, ili mwanafunzi aweze kuwa na uwezo wa kutunza vema mambo anayosoma na kufundishwa na waalimu wake darasani lazima aweze kuiongezea akili yake uwezo wa kutunza kumbukumbu kwa kufanya yafuatayo: 1 . LISHE BORA Ni wazi kuwa wengi wetu tunafahamu maana ya lishe bora, lakini kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Chuo cha American Academy of Neurology kinachojihusisha na mambo ya neva, ulibaini kuwa machungwa, Spinachi, Karoti, brokoli (aina fulani ya mboga kama kabichi), viazi vitamu na mboga mboga huuongezea uhai ubongo na kumfanya mwanadamu asiweze kushambuliwa na magonjwa wa kupooza. Aidha matunda na vyakula vyenye vitamini B, Foliki Asidi (folic acid), Niasini (niacin) Kalkumini (curcumin) husaidia kuufanya ubongo uwe na mawasiliano ya kutosha na viungo vingine vya mwili na kupunguza kwa asilimia 11 uhalibifu wa seli ndani ya ubongo. (Utafiti wa National Research Council nchini Milan, Italy unathibitisha kuwa vyakula vyenye Vitamini C na E hupunguza kiwango cha usahaulifu) 2. MAZOEZI YA MWILI Ufanyaji wa mazoezi ya mwili huimarisha misuli na kusaidia akili kuweza kufanya kazi vema, hii inatokana na ukweli kwamba tunapofanya mazoezi tunakuwa tunaongeza msukumo wa damu mwilini na hivyo kuufanya ubongo kufikiwa na damu ya kutosha ambayo ni muhimu kwa uimara wa kumbukumbu. Mara nyingi, mazoezi yanayofaa zaidi kwa afya ya mwili na uimarisha wa ubongo ni yale ya asubuhi na jioni. Kuhusu aina ya mazoezi inategemea na umbo la mtu, lakini kukimbia, kuruka kamba, kucheza mpira na hata kuinua vitu vizito vinavyolingana na uwezo wa mtu ni bora kwa afya. Mazoezi ya aina hii yakifanywa na wanafunzi yanaweza kuwasaidia pia kutunza kumbukumbu za masomo wanayofundishwa. 3 : MAZOEZI YA AKILI Ni muhimu kwa mwanafunzi kuwa na mazoea ya kuifanyisha akili yake mazoezi ya kutunza kumbukumbu kwa kuingiza kichwani mambo ambayo hakuyazoea na kuyafanyia mazoezi ya kuyakumbuka. Kwa mfano mwanafunzi anaweza kundika namba zisizopungua 14 na kuanza kuzitaja kwa kufuta mpangilio aliojiwekea. Namba zinatakiwa ziandikwe kwa kuchanganywa si kwa kuzifuatanisha kwa mtindo wa kuhesabu. Mfano, 23938393835575, baada ya kuziandika kwa mfumo huo mwanafunzi atatakiwa kuzikariri kwa dakika tano kisha kufumba macho au kutazama pembeni na kuanza kuzisoma kwa kufuata mfululizo huo, huku akihakikiwa na mtu mwingine. Mazoezi haya yatamsaidia kuondoa tatizo la kusahau na kumpa kipimo ni kwa kiwango gani hana uwezo wa kukumbuka. Endapo mwanafunzi atashindwa kufikia kiwango cha zaidi ya nusu ya namba alizojiwekea afahamu kuwa ana uwezo mdogo wa kutunza kumbukumbu hivyo anatakiwa kuongeza juhudi za kujiimarisha. Njia nyingine ya kuifanyisha mazoezi akili ni kujifunza mara kwa mara mambo mapya, ikiwa ni pamoja na kuimba nyimbo kwa lugha ya kigeni, kujifunza lugha za makabila mengine, kutembelea mitandao mbalimbali ya intaneti na kusoma, kucheza michezo ya kwenye simu na kompyuta. Aidha usomaji wa vitabu, urudiaji wa mara kwa mara wa notisi za darasani, husaidia kuongeza msukumo wa akili katika kutunza kumbukumbu kichwani. Hata hivyo tafiti nyingi zinaonesha kuwa uhudhuriaji wa majadala na uongeaji wa mambo ya msingi mbele ya watu wengi huimarisha uwezo wa mtu kukumbuka mambo kwa urahisi. 4. UTUMIAJI WA VINYWAJI Vinywaji kama kahawa, chai nyeusi navyo huchangia kuongeza uwezo wa ubongo kutunza kumbukumbu. Inashauriwa kwa mwanadamu kutumia walau kikombe kimoja cha vinywaji hivyo ili kuongeza enzymes ambazo ni muhimu kwa kuuongezea nguvu ubongo ili uweze kutunza kumbukumbu. Hata hivyo vinywaji vikali kama pombe haviruhusiwi kwani huchangia kudumaza uwezo wa kukumbuka. 5. PUNGUZA MSONGO WA MAWAZO Ubongo unaweza kushindwa kutunza kumbukumbu endapo mtu husika atakuwa na msongo wa mawazo yatokanayo na shida za kidunia. Endapo mwanafunzi atakuwa mtu mwenye kuutumikisha ubongo wake katika mawazo yenye kuumiza kila wakati, hawezi kuwa na uwezo wa kukumbuka anayofundishwa. Hivyo ni vema kupunguza mawazo kwa kuwashirikisha wengine magumu unayokutana nayo maishani na kukubali kuyaacha yapite ili yakupe nafasi ya kuishi kama wewe. Hatari ya msongo wa mawazo ni kuongeza kiwango cha seli za cortisol ambayo huharibu ubongo wa kati ambao ni muhimu kwa kutunza kumbukumbu. 6. KULALA Watu wengi wakiwemo wanafunzi wamekuwa wakipuuza usingizi kwa kusoma sana usiku na kuacha kupumzisha miili yao kwa kulala, jambo ambalo hili ni hatari kwa utunzaji wa kumbukumbu kichwani. Ifahamike kuwa usingizi ni kama chujio la akili ya mwanadamu, ambapo mtu anapolala mchakato hufanyika akilini kwa kuyachambua mamilioni ya mambo ambayo mhusika aliyaona, kuyasikia, kuhisi na pengine kuyatenda. Mchakato huo huweza kuchuja mambo mabaya na kuyatupa na mema huhifadhiwa kwenye kumbukumbu. Hivyo, kama mwanafunzi hatolala, mambo yote yakiwemo ya kipuuzi aliyofanya mchana yatabaki kwenye akili yake na kama mtindo huo wa kutolala utaendelea unaweza kuufanya ubongo uchoke na kupoteza kumbukumbu ya mambo muhimu yakiwemo ya shuleni. Utafiti uliofanywa mwaka 2008 na Chuo cha Pennsylvania ulionesha kuwa wanafunzi wanaolala kwa saa 6 kwa siku huwa na kumbukumbu nzuri zaidi ya wale wanaolala kwa kiwango cha chini ya saa hizo. Utafiti wa aina hii ulifanywa pia na Chuo Cha Luebeck na kubainisha kuwa akili huongezewa uwezo mara tufu kwa kutunza kumbukumbu pale mtu anapokuwa analala usingizi mnono. 7. TUMIA MUZIKI Muziki unatajwa kuwa na faida katika kumsaidia mtu kukumbuka mambo yaliyopita, inawezekana kabisa kwa kupita wimbo ukakumbuka mambo ambayo uliyafanya siku za nyuma. Hivyo kuufurahisha mwili kwa kucheza muziki, kusikiliza nyimbo, kunaweza kuongeza uwezo wa mtu kukumbuka mambo. Hata hivyo kujifunza lugha au jambo fulani kwa njia ya wimbo ni rahisi kukumbuka kuliko kuhifadhi maneno yenyewe. 8. KUANDIKA Ni muhimu kwa mwanafunzi kuwa na kumbukumbu za pembeni nikiwa na maana ya maandishi ya mkono. Ni muhimu kuorodhesha mambo ambayo umekusudia kuyafanya au yalikutokea kwa kuyaandika kwenye kitabu kidogo cha kumbukumbu. Mfano, unaweza kuandika siku uliyoanza shule, uliyozaliwa, tarehe uliyomaliza darasa la saba n.k. 9. ONDOA HOFU Kuna wanafunzi wengine hushindwa kukumbuka mambo si kwa sababu akili imesahau, bali wanajichanganya kwa hofu na kutojiamini kwamba wanachokumbushwa na akili kwa wakati huo kiko sahihi. Hivyo ni wajibu wa mtu kujiamini na kutupilia mbali wasi wasi wote unaojitokeza wa kuhofu kuchekwa au kutofanya vizuri katika jambo lililopo mbele yake. 10. AFYA Jambo la mwisho ambalo ni muhimu katika uimarishaji kumbukumbu za kichwani ni mtu kuwa na afya kwa maana ya kuhakikisha kuwa anatibiwa magonjwa yake na anakuwa mfuasi mzuri wa huduma za kitabibu kwa ajili ya kuuwesha mwili wake ufanye kazi kama unavyokusudia.

12 comments:

  1. Do vi2 vingine vigumu kupata nixhid

    ReplyDelete
  2. Enter your comment...safi sana, nimeipenda hii. nikweli binadam tunajisahau sana. hata swala la mazoezi tu linatushinda. asante kwa kutukumbusha.

    ReplyDelete
  3. Thanks
    Hiyo swala limenigusa sana, nilipokuwa naishi home nilikuwa naweza kusoma kitini chenye page zaidi ya 200 ndani ya Masa mawili hadi GPA zangu zilikuwa nzuri lakini tangu nianze kufanya kazi na kujitegemea nasoma pamphley siku nzima

    ReplyDelete
  4. Thanks
    Hiyo swala limenigusa sana, nilipokuwa naishi home nilikuwa naweza kusoma kitini chenye page zaidi ya 200 ndani ya Masa mawili hadi GPA zangu zilikuwa nzuri lakini tangu nianze kufanya kazi na kujitegemea nasoma pamphley siku nzima

    ReplyDelete
  5. Nina ndoto za kugundua kitu kupitia sanyansi yangu ninayoisoma,sasa basi mambo kama haya ni mhimu sana kwangu...asanteni sani

    ReplyDelete

  6. Thanks: The lesson is so better:

    ReplyDelete
  7. Ubarikiwe kwa msaada ulioutoa kwa jamii

    ReplyDelete